July 11, 2014

WAKIMBIZI SITA WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIEZI SITA AU FAINI YA SHILINGI ELFU THELATHINI KILA MMOJA


Baadhi ya wakimbizi wa makazi ya Ulyankulu wakitoka kwenye Chumba cha Mahakama ya hakimu mkazi baada ya kusomewa hukumu ya kifungo cha miezi sita jela au kulipa faini ya shilingi ya elfu thelathini kila mmoja
Na mwandishi wetu Tabora.
Watu sita ambao ni wakimbizi katika makazi ya Ulyankulu wamehukumiwa kutumikia adhabu ya kifungo cha miezi sita au kulipa faini ya shilingi elfu thelathini kila mmoja baada ya kupatikana na makosa ya kutoroka eneo la makazi ya wakimbizi Ulyankulu pamoja na kukutwa wakifanya shughuli za kiuchumi kinyume na kifungu cha makosa ya uhamiaji nchini.
Watu hao sita ambao walifikishwa kwa mara nyingine katika makahama ya hakimu mkazi mkoa wa Tabora ambapo wakili wa upande wa mashtaka Bw.Salehe Mgeni aliieleza mahakama kuwa mnamo tarehe 25 machi mwaka huu wakimbizi hao walikamatwa wakiwa wanafanya kazi ndani ya hifadhi ya msitu wa Ugalla katika Tarafa ya Ussoke wilaya ya Urambo, kosa ambalo liliunganishwa na lile na kutoka nje ya eneo la makazi ya Ulyankulu bila kibali cha Mkuu wa makazi.

Pamoja na kosa hilo la kwanza la kujihusisha na shughuli za kiuchumi kiunyume cha sheria ya Uhamiaji nchini washitakiwa hao sita walikiri makosa hayo mbele ya hakimu mkazi mkoa wa Tabora Bw.Jackton Rushwela na hivyo kuhukumiwa adhabu ya kifungo cha miezi sita au kulipa faini ya shilingi elfu thelathini kila mmoja.

Aidha wakimbizi hao waliohukumiwa ni Mapili John,Jeremia Matoli,Kitenge Sayumba,Obed Ndabasigiye,Enock Sayumo na Zarubali Sanzugwimo ambao walikamatwa katika msitu huo wa hifadhi Ulyankulu walikuwa wakifanya shughuli za uchanaji wa mbao.


No comments:

Post a Comment