June 22, 2014

Kauli ya Uganda baada ya kuwekewa vikwazo na Marekani kwa kupinga ushoga



Kauli ya Uganda baada ya kuwekewa vikwazo na Marekani kwa kupinga ushoga

Katibu mkuu wizara ya mambo ya nje wa Uganda, Balozi James Mugume, 
amesema kuwa Uganda haitishwi na vikwazo ilivyowekewa na Marekani kama 
hatua ya kupinga sheria yake kali kuhusu Ushoga.Kwa mujibu wa BBC, 
Balozi Mugume ameelezea kuwa serikali ya Uganda hata hivyo itafanya 
mazungumzo na Marekani ili kufafanua hatua waliyochukua.Amesisitiza 
kuwa wataieleza Marekani sheria hiyo inapinga tabiaambayo sio ya 
kiafrika na maadili ambayo hayakubaliki katika jamii nyingi za 
kiafrika.Serikali imesisitiza kuwa vikwazo hivyo havitakuwa na athari 
kubwa kwa nchi hiyo na pia imekanusha madai ya mashirika ya kijamii 
kuwatayari sheria hiyo imechochea ongezeko la dhuluma dhidi ya wapenzi 
wa jinsia moja


No comments:

Post a Comment