May 18, 2014

BARCELONA YATEMESHWA UBINGWA NYUMBANI KWAKO, KOCHA WA ATLETICO MADRID AWEKA HISTORIA YA AJABU ...wa Barcelona abwaga manyanga

Decisive moment: Diego Godin (second left) scored Atletico's equaliser in their 1-1 draw on Saturday
BARCLONA imevuliwa taji la La Liga kwenye uwanja wao wa nyumbani Nou Camp baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Atletico Madrid katika mchezo wa mwisho wa ligi kuu ya Hispania.
Wakiwa wanahitaji ushindi ili kutetea taji lao, Barcelona wakashindwa kulinda bao lililofungwa na Alexis Sanchez dakika ya 30 baada ya Diego Godin kusawazisha pale ilipotimu dakika ya 49.
Barcelona striker Alexis Sanchez celebrates after scoring a goal
Joy: Atletico's Diego Godin (left) celebrates his goal against Barcelona
Kwa sare hiyo, Atletico Madrid wamekuwa mabingwa wapya wa Hispania, ikiwa ni mara ya kwanza baada ya miaka 18.
Kocha wa Barclelona Gerardo "Tata" Martino amesema anabwaga manyanga baada ya kuwa na msimu mbovu.
Bowing out: Gerardo Martino will exit Barcelona after just one season in charge
Kocha huyo anatimka akiwa ameikochi timu hiyo kwa msimu mmoja tu. Anasema yeye na Barcelona wamefikia muafaka wa kusimamisha 'kibarua' chake.
Wakati Tata anatangaza kubwaga manyanga, kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone anajiwekea historia ya aina yake baada ya kuipa ubingwa timu hiyo kama alivyofanya miaka 18 iliyopita akiwa mchezaji.
High jinks: Atletico's coach Diego Simeone is thrown in the air by his players
Wachezaji tegemeo wa Atletico Diego Costa na Arda Tura walitolewa kipindi cha kwanza baada ya kuumia. Costa alibubujikwa machozi kwenye benchi baada ya kushindwa kuendelea na mchezo.

No comments:

Post a Comment